Friday, March 15, 2013

PENNY~ NEW MAMA KIJACHO IN TOWN, ADONDOSHEWA ZAWADI YA GARI

 
 
 
 
Mapenzi ya Diamond na Penny sasa yameenda next level kwani sasa wanatarajia kuitwa mama na baba nanilihu miezi michache ijayo, yote hayo yamejulikana katika kipindi cha XXL ya Clouds Fm na Gossip Cop ambapo Diamond alisema ni kweli Penny ambaye ni mtangazaji wa DTV ni mjamzito na wanatarajia kupata mtoto,

Soudy Brown alimuuliza kuhusu fununu za kutumia Milioni 15 kununua gari la mke wake mtarajiwa Penny

Diamond amekiri kwamba ni kweli kamnunulia Penny gari kwa sababu anaelekea kuwa mama watoto ambapo namkariri akisema “nilimuuliza gari gani anapenda, nimemuagizia iko njiani inakuja siwezi kusema ni bei gan ila kwa sasa anatumia la muda wakati akisubiria gari lake”

Alipoulizwa kuhusu kumuoa na kama mtoto atazaliwa nje ya ndoa, Diamond amejibu “siwezi kusema lini ila Mwenyenzi Mungu ndio anajua inaweza ikawa harusi ila kuna time inafika inabidi utulie, siwezi kusema chochote kwa sababu inawezekana mtoto akazaliwa ndani ya ndoa pia “

No comments:

Post a Comment