Friday, February 1, 2013

GIRLS SOMA HAPA!!!

Yaani Wanawake kwa kupenda Pete dah,Mungu awasaidie. Mtu una ndoto zako maskini, kubwa tu, Mungu kakupa akili nzuri tu, ila anatokea mtu from nowhere, wala hata sio type yako, humpendi kiivyo, ila kisa kaja na Ring basi mnasisimka kama mmeguswa na Jini Subiani.

Akishakupa mpete wa bati akasema; 'Honey, ntakuoa', yaani mnakuwa kama mmepigwa nusu kaputi za Maternity Room, mnayeyuka kama Koni za Azam, unasahau kabisa kila ndoto uliyonayo, Unamkabidhi Tunutu alinde shamba la uwele!

Kuna girls wameolewa na watu wasio sahihi wameua ndoto zenu za kusoma, mlikuwa mnataka mjiendeleze Jamaa halitaki, linakuuliza unasoma ili iweje?? Unataka unizidi kipato, Myopic Brained-husband! Na wengine wakiona tu umejaza fomu za Chuo Kikuu wanakulia timing wanakutundika mimba, ukiwaza kuweweseka na Kitumbo cha ujauzito na kufanya assignment za class, mwenyewe una-surrender, una-forego Elimu kisa pete, ujuha huo!

Girls, msiue ndoto zenu kisa umeahidiwa Pete na juha moja lisilotambua Priorities zako, kama anakupenda ataku-support positively on ur plans, huyo ndo mume, kama umeplan kusoma, soma kwanza, pete zipo! Kama umeplan kujenga jenga kwanza usikimbilie ndoa utageuzwa Incubator kutotoa mfululizo na hata veranda hutamaliza... Pete ni mbati tu wa duara usiharibu akili zenu, Ur dreams come first, Pete si uchonge hata mwenyewe kwa sonara Mwenge?? WanaaumeTumeshajua mnapenda sana pete, tunawavisha, na tutawavisha sana hadi viunoni kama shanga, mnakuwa watumwa wetu kiulaini!

WAKE UP!!!



SOURCE: SETH DE JESUS GIOVANN


No comments:

Post a Comment